Access Kiswahili Sahili GD4 (Approved)


Kiswahili Sahili, Gredi ya 4, ni kitabu kinachompa mwanafunzi fursa nzuri kutangamana na Mtaala wa Kiumilisi kupitia 
mada na shughuli alizoandaliwa. Lengo hasa la mtaala huu mpya ni kumwezesha mwanafunzi kupata maarifa pamoja na kumjengea 
umilisi mzuri wa masuala na maaarifa mbalimbali ili aweze kuyatumia katika maisha yake ya kila siku.
Kitabu hiki kinampa mwanafunzi nafasi ya kujenga umilisi wake katika lugha ya Kiswahili kupitia stadi zilizoshughulikiwa 
humu.Kitabu hiki kinashughulikia kusikiliza na kuzungumza kwa namna inayomwezesha mwanafunzi wa Gredi ya 4 kujenga 
matamshi, kutumia lugha vizuri kulingana na muktadha. Sehemu ya kusoma inampa mwanafunzi mbinu za kusoma kwa ufahamu, 
kusoma kwa kina na kusoma kwa mapana na hivyo kumwezesha kujenga ufasaha wake, wa lugha. Kitabu hiki kinaangazia 
stadi ya kuandika ambapo mwanafunzi anaongozwa hatua kwa hatua jinsi ya kuandika tungo za namna mbalimbali. 
Sehemu ya sarufi inampa mwanafunzi fursa ya kujenga umahiri wake wa kutumia lugha kwa ufasaha.
 

ISBN: 9789966194503 SKU: 2010127000837
KES 620
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect