Bustani ya Edeni
Bustani ya Edeni ni riwaya tamu inayorejelea mazingira yajana, leo na kesho yaliyoghasiwa na binadamu kwa tamaa / na uchu wa kuumba huku nguvu zake zikiumbua. Usafi unajikunja na uchafu unajikunjua; maji hayanyweki, hewa haivutiki, chakula hakiliki - yote haya kwa pupa ya maendeleo.Kisha'Franco'; ngozi kuchubuka, vichwa kuwanga, miti kukauka na serikali jicho kafumba. Jitihada za Jonalisti zinapigwa vita moto mmoja.Pasta yona wa yona anajitoa mhanga kwa damu na uhai kuokoa hali hii, tayari propaganda imekolea magazetini, redioni, vikaoni kanisani, propaganda ya kuufumba umma macho... kweli mam bo yametumbukia nyongo.Hii ni riwaya yenye kusuta na kuvuta fikira na kila mmoja ataisaka.Profesa Emmanuel Mbogo ni mhadhiri wa fasihi mwenye mkono mpevu katika uandishi.