Kamusi Mwafaka kwa Shule za msingi


Kamusi Mwafaka kwa Shule za Msingi itawafaa sana wanafunzi wa shule za msingi kuelewa maana na matumizi ya maneno wanayokumbana nayo katika Kiswahili cha kiwango chao. Pia, kamusi hii imetayarishwa kama kitabu cha kutumiwa katika kufundisha na kusoma lugha ya Kiswahili darasani.Maneno katika kamusi hii yamechaguliwa kwa uangalifu. Haya ni maneno ambayo mwanafunzi hukumbana nayo mara kwa mara katika maisha yake ya kila siku, popote alipo. Isitoshe, maana ya maneno hayo yameelezwa kwa urahisi sana. Kila neno limefuatiwa na tafsiri yake katika Kiingereza, wingi wake, aina ya neno husika, maana yake na matumizi katika sentensi.Michoro mingi imeandamana na maelezo ili kusaidia mtumiaji kuelewa maana ya maneno magumu kwa urahisi.

KES 951
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect
Author Moran
ISBN 9789966347787
SKU2010127000577

Reviews

Leave a product review
or cancel