KLB Skillgrow Mazoezi ya Lugha Hatua ya 1

by Sheila Wandera, Susan Mukundi, Phillip Lumwamu, Mutahi Miricho, Diana Madara


KLB Skillgrow Mazoezi ya Lugha Hatua ya Kwanza (Kaaba cha Mwanafunz0 ni kitabu mojawapo kati ya vitabu vinavyochapishwa na Kenya Literature Bureau vya msururu wa Skillgrow. Msururu huu wa vitabu umezingatia Mtalaa wa kiumilisi wa mwaka wa 2017 wa masomo ya shule za Nasari. 

Kitabu hiki kimekusudiwa kumwezesha mwanafunzi kukuza uwezo wa kutumia stadi zote nne za lugha ya Kiswahili; Kusikiliza, Kuzungumza, Kusoma na kujiandaa Kuandika. Kupitia stadi hizi, mwanafunzi anakuza uwezo wake wa lugha. 

Toleo hili limejumuisha mambo muhimu ambayo yanachangia ujifunzaji wa sasa ambayo ni masuala mtambuko, maswali dadisi, masuala ya jinsia, picha murua za kuchangamsha na kuibua hamu ya kudadisi kwa mwanafunzi na mbinu tofauti za kumwezesha mwanafunzi kukuza uwezo wake wa kujifunza. Mazingira halisi ya mwanafunzi yamezingatiwa katika kukuza kazi hii. Hili linamwezesha mwanafunzi kujifunza katika hali halisi. Lugha sahili imetumika ili kurahisisha kuelewa kwa mada zote katika kitabu hiki. 

ISBN: 9789966651884 SKU: 2010127000705
KES 278
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect

Reviews

Average rating: 5

from 1 review

5 1 five star review
4 0 four star reviews
3 0 three star reviews
2 0 two star reviews
1 0 one star reviews
Add your review
Add your review