Maji Shingoni
by Geranija
Prof. KITHAKA WA MBERIA anafundisha Isimu, Kiswahili na Mawasiliano katika Chuo Kikuu cha Nairobi.
Mbali na kufundisha, anajishughulisha na utunzi wa mashairi na tamthilia na pia uchoraji.
Kwa muda mrefu ameshiriki kama mwamuzi katika Tamasha za Muziki za Kenya, Tamasha za Muziki na Utamaduni za
Kenya na Tamasha za Uigizaji za Shule na Vyuo za Kenya. Yeye ni mwanakamati wa Kamati ya Kitaifa ya Tamasha za
Muziki na Utamaduni za Kenya na vili vile mwanakamati wa Kamati Kuu ya Chama cha Waandishi cha Kenya.
Vitabu vingine vya Prof. KITHAKA WA MBERIA ambavyo vimechapishwa na Marimba Publications Ltd. ni Natala(1997),
Mchezo wa Karata(1997), Kifo Kisimani(2002), Maua Kwenye Jua la Asubuhi(2004) na Radio na Mwezi(2005).