Pango

by K W Wamitila


Pango ni tamthilia inayotufunulia na kujadili utata wa kisiasa, uchumi, uongozi na migongano ya wimbi la ukale na la usasa. Ni kichokozi na kichocheo cha fikra kwa wahakiki na wanafunzi vyuoni na katika shule za sekondari. Mwandishi ni mweledi wa lugha na kunga za fani ya tamthilia. Tamthilia hii ni mchango mwingine mwafaka katika medani ya fasihi hasa uga wa drama. Kwa mara nyingine tena, Wamitila amedhihirisha ukereketwa wake katika kuikuza na kuitilia mbolea fasihi ya Kiswahili hapa Afrika Mashariki.

ISBN: 9789966882882 SKU: 2010143000003
KES 377
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect