Queenex Chakula cha Biko na Hadithi Nyingine 1C

by Pauline Kea


Queenex hadithi za ziada ni msururu wa hadithi zinazofuata mfumo mpya wa elimu. Mfumo huu wa elimu unadhamiria kuhakikisha kuwa matokeo ya mafunzo ni ujenzi wa umilisi utakaomwezesha mwanafunzi kutumia ujuzi wake kujiendeleza shuleni, nyumbani na katika jamii.
Kitabu hiki ni cha wanafunzi wa Gredi ya kwanza na kimejumuisha hadithi za kusisimua, picha za kuvutia na msamiati. Hadithi hizi zitamwezesha mwanafunzi kukuza maadili, umilisi wa lugha na pia kuelewa masuala mtambuko. Mada kuu zilizozingatiwa katika kitabu hiki ni:
- Usafi wa mwili 
- Usafi wa mazingira 
- Vyakula vya kiasilia 
- Shuleni

ISBN: 9789966141132 SKU: BK00000002309
KES 290
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect