Spotlight Kurunzi ya Kiswahili Grade 4 (Approved)

by Matei


Kurunzi ya Kiswahili Kitabu cha Mwanafunzi Gredi ya Nne kimeandaliwa kwa ustadi ili kumwezesha mwanafunzi kumudu mtaala huu unaolenga umilisi kwa nijia sahili, yenye mvuto na ya kumjumuisha moja kwa moja kwenye shughuli za ujifunzaji.

Kitabu hiki:

* Kimeshughulikia mada kwa namna ambayo inamwezesha mwanafunzi kushiriki kikamilifu katika ujifunzaji.

* Mada na shughuli za ujifunzaji zimeteuliwa kwa uangalifu ili kumjengea mwanafunzi umilisi wa aina mbalimbali.

* Kina mazoezi na mijarabu anuwai ya kumtathmini mwanafunzi.

* Kina picha halisi na michoro ya kuvutia inayosaidia katika uelewa wa mada.

* Kinalenga kumsaidia mwanafunzi kutumia vifaa vya teknolojia kama vile video, redio na tabuleti katika kurahisisha ujifunzaji.

*  Mbinu tofauti za ujifunzaji zimejumuishwa kama vile kazi mradi, shughuli nje ya darasa, kumwalika mgeni, kutumia nyimbo, mashairi, kumhusisha mzazi au mlezi, uchoraji na ujifunzaji katika vikundi. Mbinu hizi zinasaidia kuujenga umilisi wa mwanafunzi.

* Mada na shughuli za ujifunzaji zimeshughulikia masuala mtambuko na kumsisitizia mwanafunzi maadili.

* Kitebu cha mwalimu kipo ili kumpa mapendekezo katika ufunzaji.

ISBN: 9789966572165 SKU: 2010127000813
KES 563
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect