Safari ya Peponi
by Queenex
Mimi Bendera ni kijana wa familia tajiri na tunaishi jijini. Baba yangu Mzee Mwinyi Mapesa ameahidi kunipeleka mahali fulani anapopasifia sana paitwapo Peponi iwapo nitafanya vyema masomoni, jambo ambalo ninamuahidi nitalitimiza. Baada ya kuhamia mashambani, natunga urafiki na kijana anayeitwa Makata. Makata ni kijana safihi na mtundu ajabu. Ninapomtajia kuhusu Peponi, kumbe anapajua! Kwa kuwa baba amekawisha ahadi yake, Makata ana mpango wa kunipeleka Peponi na safari inaanza. Ni safari ndefu inayotulazimu tuvuke mpaka wa nchi. Je, Peponi ni wapi hasa? Ni mahali pa dhana ama ni pa ukweli na ni nini hasa cha mno kilicho huko Peponi? Je, nitafikishwa Peponi na Makata au na baba? Je, baba yangu ananipenda kuliko ndugu zangu jinsi anavyonisisitizia? Upo uhusiano gani baina ya baba, Ngoma na genge lake?