Shisia reviewed on 28 Apr 2021
Makovu Ya Uhai
Misururu ya masaibu yanayomwandama Daudi Marefu ni tele. Anapoibuka kwa hili anazamishwa kwa lile. Ndoa yake inatibuka. Anapigwa kalamu. Anapodhani kuwa nyota ya jaha imemwangazia, mwanawe wa pekee anafariki dunia. Haya ni masuala mazito kumkabili mtu mmoja kwa mkupuo. Kwanini mwanadamu hupitia mitihani maishani? Kwanini ndoa zinavunjika ndivyo sivyo? Mwandishi anajaribu kuyajibu masuala yale kupitia matukio aliyoyasuka kwa umbuji kwenye kazi hii; Makovu ya Uhai