OUP Kiswahili Dadisi Grade 5 Kitabu cha mwanafunzi (Approved)

by J. Ndege, P. Kea, E. Osoro, Z. Mucheria


Kiswahili Dadisi ni msururu wa vitabu vipya vilivyoandikwa kwa njia ya kipekee ili kutosheleza mahitaji ya mtalaa wa umilisi. Vitabu hivi vitamwezesha mwanafunzi kupata ufahamu wa lugha kupitia stadi za kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika, na vilevile sarufi. Aidha, vina mazoezi murua ambayo yatampa mwanafunzi hamu ya kujifunza. Pia vinakuza umilisi uliopendekezwa, maadili na kufahamisha kuhusu masuala ibuka. 
Katika Kiswahili Dadisi, Kitabu cha Mwanafunzi, Gredi ya 5, utapata: 
• mada zilizopangwa kwa kuzingatia muainisho wa mtalaa mpya. 
• mifano halisi ya miktadha ambapo lugha hutumika. 
• mazoezi ya kuwahamasisha wanafunzi kuendeleza ujifunzaji nje ya darasa na yale yenye kuwashirikisha katika shughuli za
kijamii zinazokuza ujifunzaji. 
• mazoezi yanayomhusisha mwanafunzi moja kwa moja.
• jinsi ya kuwashirikisha wazazi na walezi ili kuimarisha uwajibikaji. 
• vifungu vya kumburudisha na kumfikirisha mwanafunzi katika sehemu ya 'Burudika'. 
Kiswahili Dadisi, Kitabu cha Mwanafunzi kina Mwongozo wa Mwalimu ambao pia una mazoezi na maelekezo tosha ambayo mwalimu atahitaji ili kumwongoza mwanafunzi aweze kufaulu katika mtalaa huu wa umilisi.

ISBN: 9780195749052 SKU: BK00000001678
KES 563
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect