Vitendawili kwa mashairi 5b
Vitendawili kwa mashairi 5b ni kitabu kinachonuiwa kuendeleza msingi wa kusoma na kukuza uwezo wa kusoma wa wanafunzi wa
Darasa la Tano katika shule za msingi. Miongoni mwa sifa za kipekee za kitabu hiki ni:
Mashairi mepesi ya tarbiya ya beti moja moja. Umahiri wa mtunzi wa kutoa majibu ndani ya beti. Mtindo maalumu wa
kutega na kutegua vitendawili kwa njia ya mashairi. Kuwapitisha na kuwalea wanafunzi katika mazingira ya chemsha
bongo au vitendawili ili kukuza na kupanua fikra zao. kurahisisha ufahamu ili kupata jibu la kila kitendawili kwa
kuunganisha herufi au silabi fulani zilizomo ndani ya kila ubeti pamoja na kupitia picha zenye kusisimua na zenye rangi za
kupendeza. Mradi wa kusoma ni mfululizo wa vitabu vya ziada unaoambatana na kozi ya Kiswahili Sanifu. Vitabu vingine
katika kiwango hiki ni: 5a Embe tamu 5c Ndoto ya Riziki