Moran Stadi za Kiswahili - Mwanafunzi Gradi 5 (Approved)


Stadi za Kiswahili ni mfululizo wa vitabu vya kiada vya Kiswahili vilivyoandaliwa kwa kufuata Mtaala wa Umilisi. Kitabu hiki kina sifa kuu zifuatazo: 
• Kimeandikwa kwa Kiswahili cha kiwango cha mwanafunzi wa Gredi ya 5. 
• Maswali dadisi yametumiwa kutanguliza dhana zilizomo. 
• Kimejumuisha shughuli za mwanafunzi binafsi, shughuli za wanafunzi wawiliwawili na za makundi ya wanafunzi. 
• Kimeshughulikia masuala makuu yote kwa mujibu wa ruwaza ya Kiswahili cha Gredi ya 5
• Kimejumuisha mada kuu na mada ndogo zote. 
• Yaliyomo yamepangwa kulingana na ruwaza ya Kiswahili cha Gredi ya 5. 
• Yaliyomo yamewasilishwa kwa ubunifu wa kiwango cha juu. 
• Kimeshughulikia matokea maalum yanayotarajiwa katika Gredi ya 5. 
• Kimejumuisha umilisi wa kimsingi kwa mujibu wa Mtaala wa Umilisi. 
• Kimeshughulikia masuala mtambuko yote. 
• Yaliyomo yanakuza maadili yanayopendekezwa katika Mtaala wa Umilisi. 
• Shughuli za ujifunzaji zinakuza stadi za kusikiliza na kuzungumza, kusoma na kuandika 
• Michoro na picha za rangi zinachangia yaliyomo kueleweka kwa urahisi. 
• Maandishi makubwa na ya rangi mbalimbali yanasomeka kwa urahisi. 

Haya na mengine mengi yanadhamiriwa kumwezesha mwanafunzi wa Gredi ya 5 kuwasiliana kwa Kiswahili sanifu katika mazingira mbalimbali.

KES 592
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect