Maumbile si Huja


...Amina aliingia ukumbini alimokuwa Juma. Damu ilikuwa ikimwenda mbio. Hata hivyo Juma hakumkaripia kama alivyodhani. Alimtazama kutoka miguuni hadi nyweleni. Na alifanya hivi kwa dharau huku ameinua pua lake. Mara akamwambia Juma ni tajiri mkubwa na tena mbaguzi. Anaamini kwamba Mwarabu ni mwanadamu bora kuliko wanadamu wa usuli mwingine. Itikadi hii, pamoja na taasubi zake za kiume, ndiyo mambo ambayo yanamletea maangamizo hatimaye. Mkewe Juma, Amina, anajiona ni mdhulumiwa na anashirikiana na Said, ambaye ni mtumishi, iii kumwadhibu Juma kwa kumfilisi. Hadithi hii inasisimua kwa undani wa hisia na mahusiano halisia ya wahusika. Lakini kinacho-vutia zaidi ni ule msuko na msokoto wa vitushi hivi kwamba vimepangwa kama punje za shanga kwenye ukambaa wake.

KES 447
International delivery
Free delivery on orders over Ksh 2,000
Free click & collect
Author John Habwe
ISBN 9966223878
SKU2010143000033

Reviews

Leave a product review
or cancel